Archive for November, 2005

Bendera ya Uingereza yafanyani katika tovuti ya CHADEMA?

November 23, 2005
Ndesanjo amekuwa akipigia kelele matumizi ya lugha ya kiingereza katika tovuti za kitanzania. Sasa leo katika kuipitia tovuti ya CHADEMA nimeona wameweka bendera ya Uingereza juu kabisa kwenye tovuti yao. Hiyo bendera inafanya nini hapo? Mimi sijuhi sababu labda kama kuna anayefahamu anisaidie.

UKIMWI bado ni tishio

November 22, 2005
Shirika la umoja wa mataifa linaloshughulikia UKIMWI, UNAIDS kwa kushirikiana na Shirika la Afya duniani, WHO limetoa taarifa ya mwaka inayoonyesha jinsi UKIMWI ulivyo bado ni tishio hasa Afrika kusini mwa jangwa la Sahara. Unaweza kuisoma taarifa hiyo kwa kubonyeza hapa

Kiswahili kitolewe utumwani kwanza

November 18, 2005
Jeff Msangi kaanzisha mjadala wa kiswahili katika blogu yake. Ametoa hoja za msingi ambazo zaweza kujadiliwa. Ili mjadala ule unoge naongezea makala iliyoandikwa na Prudence Karugendo anayetoa hoja kwamba tuanze kukitoa kiswahili utumwani kwanza. Hoja yake ni kwamba kiswahili kimeazima maneno mengi sana ya kiarabu wakati tuna lugha kwa mamia za kibantu ambazo tungeweza kutumia maneno yake na kubadilisha mengi ya kiarabu. Soma makala yake hapa na mjadala uendelee.

Uvutaji na unywaji wa pombe na Saratani tena

November 18, 2005
Engidio amesema kwamba kuna watu wametishwa sana na habari niliyoiweka hapa kuhusu unywaji pombe na Saratani. Sasa naweka kiungo kingine kuonyesha msisitizo wa jambo hili tena. Soma Hapa uone mambo zaidi kuhusu pombe sigara na saratani.

Saratani yazidi kuongezeka shauri ya kubwia pombe

November 16, 2005
Soma habari hii inayotoa onyo juu ya ongezeko la saratani kutokana na kunywa kupindukia. Bonyeza hapa

Uhuru si urithi

November 15, 2005

Nimekutana na nukuu hii:

“No people are really free until they become the instrument of their own liberation. Freedom is not a legacy that is bequeathed from one generation to another. Each generation must take and maintain its freedom with its own hands.” By John Henrik Clarke

Kila kizazi inabidi kipambane kujipatia uhuru wake.

Makala za Prudence

November 13, 2005
Mzalendo mmoja aitwaye Prudence Karugendo amenitumia makala zake ambazo angependa zisomwe na watanzania wengine ili kubadilishana mawazo na kuleta changamoto katika kujadili mustakabali wa nchi yetu. Nimeweka kona ya makala zake kwenye blogu hii chini ya Kona ya Padre Karugendo. Hawa ni watu wawili tofauti. Mmoja ni Privatus mwingine ni Prudence. Kwa leo naweka makala zake tatu. Moja inaitwa kiini macho cha kusamehewa madeni. Pamoja na mambo mengine anaongelea misamiati migumu inayotumiwa katika kuandika mambo ya kiuchumi. Anahoji pia kwa nini tunaambiwa sasa tusherehekee kusamehewa madeni wakati ambao hatukuambiwa yalikopwa lini, na nani, kwa ruhusa ya nani na yalifanyia nini? Isome hapa. Nyingine mbili zinahusu amani. Moja anauliza kama kweli Tanzania kuna amani au ni kiini macho cha amani. Isome kwa kubofya hapa. Nyingine anauliza je ni upinzania au chama twawala kinachohatarisha amani? Isome hapa

Tanzania yaingizwa kwenye kapu la Misaada mingine ya Marekani

November 11, 2005
Tanzania imefanikiwa kuingizwa katika mpango wa misaada wa Marekani unaoitwa Millenium Challenge Corporation (MCC). Ili uingizwe humo ni lazima kwanza uwe na utawala bora kwa vigezo vya jamaa wa Benki ya Dunia na Wizara ya Fedha ya Dunia (International Ministry of Finance), wenyewe wanaita International Monetary Fund. Sasa tungoje majivuno na matusi toka kwa mwenyewe. “Wale wote mnaosema nchi haina utawala bora ni vipofu. Hamuoni hata Marekani inatambua? Nyie watanzania msioona ni watu wa ajabu sana”. Tutayasikia haya karibuni. Soma Hapa habari hiyo.

Wanywaji wa Kahawa Huree

November 9, 2005
Tafiti zinachanganya Kweli. Tofauti na inavyoaminika kwamba kunywa kahawa kwa wingi husababisha Magonjwa ya moyo, utafiti mpya umegundua kwamba unywaji wa Coca Cola unaweza kuwa hatari zaidi. Soma hapa

Makala kuhusu Askari kuwachapa Raia

November 9, 2005
Bwana Sakito Mallya ameandika maoni yake kuhusu Askari wa Tanzania kuwapa kipigo raia. Makala hiyo ilitoka kwenye Gazeti la Rai la tarehe 3/11/2005. Unaweza kuisoma kwa kubonyeza hapa

Design a site like this with WordPress.com
Get started