BBC iliendesha mdahalo mzuri sana kati ya Nicholas Crawford toka WFP na Tajudeen Abdul-Rahem Wa Justice Afrika kuhusu chakula barani Afrika. Jamaa wa Justice Afrika anadai kwamba hakuna haja ya Afrika kupewa msaada wa chakula na anajaribu kuelezea kiini cha tatizo la njaa barani Afrika na jinsi misaada inavyolemaza bara hili. Mzungu wa WFP anatetea umuhimu wa msaada wa chakula. Kwa kweli nakusihi usome mdahalo huo hapa. Ni mdahalo poa mno
Njaa ya Bara la Afrika ni ya kujitakia?
February 16, 2006Kuua mwenzako Ni upendo?
February 16, 2006Nchi ya Botswana imekumbwa na ongezeko la mauaji yanayotokana na wanaume kuwaua wapenzi wao. Mwaka 2005 peke yake inasemekana kulitokea vifo sabini. Wenyewe siku hizi wanaita “Passion Killings”. Botswana ni nchi ndogo- si kwa ukubwa wa eneo bali kwa idadi ya watu. Ina watu wapatao milioni moja na laki sita tuu. Halafu maambukizi ya Ukimwi ni ya kutisha. Takwimu zinaonyesha kwamba ni asilimia 40 ya watu wazima walioambukizwa. hapohapo kuna ongezeko kubwa la vifo kutokana na ajali nyingi shauri ya uendeshaji mbovu hasa kutokana na kunywa pombe kupindukia. Sasa haya mauaji ya kina dada tena inaongezea idadi ya vyanzo vikuu vya vifo yaani UKIMWI na Ajali. Ni hatari. Wanaume hawa mara nyingi wakishaua nao hujiua kwa vile wanajua watakuja kuhukumiwa adhabu ya kifo. Soma habari hiyo hapa
Ongezeko la makusanyo ya kodi
February 15, 2006Nilipokuwa napitia kwenye kibaraza cha Msaki Nimekuta mahali alipoongelea ziara ya Rais JK huko TRA. Kati ya mambo ambayo serikali ya Mkapa imeondoka madarakani ikijisifu kwamba imefanya vizuri ni ongezeko la makusanyo ya kodi. Walikuwa wakisema kwamba makusanyo yaliongezeka toka shilingi bilioni 25 kwa mwezi mwaka 1995 na kufikia bilioni 120 wakati fulani mwaka 2005. Ambacho hatukuambiwa ni ongezeko halisi. Kiuchumi ingeleta maana kama tungeambiwa hizo bilioni 125 za mwaka 2005 (miaka kumi baadaye) zina thamani gani. Kwa kweli njia rahisi ya kulinganisha mambo kama haya huwa ni shilingi bilioni 25 za mwaka 1995 zingeweza kufanya nini mwaka 2005. Kama hili halikuelezwa basi inaweza ikawa ni hadithi tuu. Pengine ukipiga mahesabu zingekuwa na thamani sawa. Jambo la pili ambalo tungefaa tuelezwe ni chanzo cha kodi hizi. Nadhani ukifuatilia utakuta mchango mkubwa unatokana na kodi ya mapato. Na kwa vile mwajiri mkuu ni Serikali basi inajilipa kodi yenyewe. Kwa jinsi ambavyo kumekuwa na tambo za ongezeko la wawekezaji basi tungetarajia kwamba “Cooporate Tax” ndiyo ingetoa mchango mkubwa katika kodi. Hilo bado halijawezekana. Kwa hivyo Changamoto iliyo nayo Serikali ya awamu ya nne ni kuziba mianya inayotumiwa na hao wawekezaji uchwara ili kuongeza “Cooporate Tax”. Vinginevyo kama hadithi hii ya ongezeko la kodi kutokana na kodi ya mapato itaendelea hatutafika mbali sana.
Maisha yetu baada ya Miaka 50
February 15, 2006NEPAD ubeberu mpya
February 15, 2006Gregory yuko wapi?
February 15, 2006Ilikuwa lazima Yesu afe?
February 15, 2006Mambo mengine! sijuhi tuanzie wapi
February 1, 2006Tumepoteza maelfu ya miaka ya elimu
January 19, 2006Vyama Viendeshwe na wanachama
January 19, 2006Ukweli ni kwamba kwanza kabisa chama ni kikundi cha watu wenye mwelekeo unaofanana au wanakubaliana kiitikadi. Kama ni kikundi basi inabidi kiendeshwe na hao wanachama. Hakuna haja ya kila mtanzania kuendelea kuendesha vyama ambavyo ni vya watanzania wachache sana. Hivi ni asilimia ngapi ya watanzania ni wanachama wa vyama vya siasa? Hili tulivalie njuga ili hii ruzuku ifutwe. Sioni kama eti ruzuku inasaidia kukuza vyama na hatimaye demokrasia. Kwanza hili suala la kufikiria demokrasia ni vyama vingi sijuhi limetoka wapi. Hata kama pesa hizi kinadharia zina lengo la kuimarisha vyama basi kinachoimarika ni kimoja tuu. Hata kama vingeimarika vyote, viimarishwe na wanachama wenyewe. Wanaopenda vyama wavichangie.
Hivi vyama vya upinzani ingebidi vianze kuchimba masuala ya msingi ambayo yanafanya CCM kuwa na uwezo mkubwa wa kifedha. Kwa mfano mali ambazo CCM ilirithi wakati mfumo wa vyama vingi ulipoanza. Angalia viwanja vya mpira kibao bado ni vya CCM, majengo mengi ambayo yalijengwa kwa kodi za wananchi bado ni ya CCM. Kwa nini mali hizo ziendelee kubaki za CCM? Tume ya Nyalali ilipendekeza kwamba mali hizo zirudishwe Serikalini lakini mpaka leo hakuna kilichorudishwa. Halafu jamaa wa upinzani wanakaa kukimbilia ruzuku ambayo kila mwaka itaendelea kuongezeka kw CCM huku ikipungua kwao, huku Chama hiki twawala kikiendelea kufaidika na mapato ambayo ni mali ya kila mtanzania. Pamoja na mambo mengine ya katiba na tume huru ya uchaguzi mimi nimeongele mambo mawili yanayohusu pesa.
Hili la ruzuku wanablogu wote tulivalie njuga. Vyama viendeshwe na wanachama hizo hela za ruzuku zikabiliane na kipindupindu au shughuli nyingine za kimaendeleo.